Dec 19, 2013

LULU AFUMWA ‘AKIDUU’ NA YOUNG D NDANI YA GARI


 
MWISHONI mwa wiki iliyopita, taarifa zilienea katika mitandao ya kijamii na vyombo mbalimbali vya habari Bongo kwamba msanii wa Bongo Fleva, David Genzi ‘Young Dee’ na nyota wa filamu, Elizabeth Michael ‘Lulu’ wamebambwa na polisi wa doria wakivunja amri ya sita ndani ya gari aina ya Hyundai, Mbezi Beach jijini Dar es Salaam, tukio lililojaa utata mkubwa. 
Kwa mujibu wa habari hizo, wawili hao walinaswa wakifanya uchafu huo na askari waliokuwa doria lakini wakawavuta chobingo na baada ya muda, wakawaachia na kutokomea kusikojulikana.
Ili kupata ukweli wa tukio hilo la aibu, paparazi wetu alianza kwa kumvutia waya Young Dee na kumsomea mashtaka yake ambapo alifunguka kuwa ni kweli amezisikia habari hizo lakini akakana kwamba ishu hiyo siyo ya kweli bali imezushwa na kundi la watu wenye lengo la kumharibia jina lake mbele ya jamii.



No comments:

Post a Comment