Waombolezaji nchini Afrika
Kusini wanaingia siku ya pili katika zoezi la kutoa heshima za mwisho kwenye
mwili wa Rais wa kwanza mweusi nchini Afrika Kusini Hayati Nelson Mandela.
Maelfu ya watu wamejipanga kwenye mistari
wakisubiri kutoa heshima zao za mwisho kwenye mwili huo uliolazwa katika ikulu
kwenye jengo la Muungano mjini Mjane wa Marehemu Graca Machel na Rais wa sasa wa Afrika Kusini Jacob Zuma, viongozi wa serikali na wanafamilia walikuwa ni miongoni mwa waliotoa heshima zao za mwisho kwenye mwili wa Marehemu Mandela siku ya jumatano.Viongozi mbali mbali pamoja na raia wa Afrika Kusini walianza kutoa heshima zao za mwisho kuanzia jumatano
Kabla ya kuwekwa katika jengo la ikulu awali mwili huo ulichukuliwa katika msafara kutoka chumba cha maiti cha hosptali hadi kwenye jengo la Muungano.
Msafara wenye jeneza la Marehemu uliondoka mjini katika Hosptali ya jeshi muda mfupi siku ya jumatano. Jeneza lilibebwa kwenye gari maalum na kufunikwa bendera ya Afrika Kusini.
Wananchi walijipanga kando kando ya barabara lilipopitishwa jeneza
Msafara ulipita katika mitaa huku baadhi ya raia wakikimbia pembeni kwenye mstari wa askari wa wanajeshi Mwandishi BBC's Joseph Winter katika mji wa
Wanajeshi waliobeba jeneza
Marehemu Mandela atazikwa nyumbani kwake katika kijiji Qunu katika jimbo la
Watu nchini Afrika ya Kusini wamekusanyika kwa siku ya pili leo kutoa heshima zao za mwisho kwa mwili wa rais wa zamani wa nchi hiyo Nelson Mandela ambao umewekwa katika jengo la makao makuu ya serikali mjini Pretoria.
Polisi wamewekwa barabarani katika gwaride la heshima wakati jeneza la Mandela likirejeshwa katika jengo hilo la serikali katika msafara maalum, baada ya kuhifadhiwa katika hospitali ya jeshi. Nje ya jengo hilo la serikali, watu walikuwa wakisubiri kuuona mwili wa Mandela kuanzia asubuhi leo. Wanajeshi walikuwa wa kwanza leo kuruhusiwa kutoa heshima zao.
Rais Jacob Zuma, mjane wa Mandela, Graca Machel, na mke wa zamani wa Mandela, Winnie Madikizela, walikuwa wa kwanza jana kuuona mwili wa Mandela, wakifuatiwa na viongozi kadha wa mataifa ya Afrika pamoja na watu wengine mashuhuri.


No comments:
Post a Comment