Dec 25, 2013

KWA MAVAZI HAYA, LAZIMA HOUSE GIRL AWE MKE BI MDOGO


Naaam Mswahili mwenzangu, leo japo kiduchu nimeona poa tuzungumze kuhusu tabia za akina mama wa mujini hasa wale ambao ni mambo safi wene tabia ya kuchukua wasichaa toka shamba na kuwaweka ndani kama ‘ma hausi geri’
 
Akina mama hao wamekuwa wakijisahau kiasi chakumpa mtumishi huyo majukumu yenye kuashiria kupitiliza. Utamkuta msichana wa kazi ndiye mpishi wa chakula cha baba siku zote, yeye ndiye anayemuandalia baba maji ya kuoga na mambo yanapozidiana msichana wa kazi hutakiwa hata kufagia na kuipamba chumba cha wazee.

SASA JIULIZE??? KAMA WEWE NI MWANAMUME MKEO HAFANYI MAJUKUMU YOOTE HAYO NA YANAFANYWA NA DADA WA KAZI NA ANAYAFANYA VIZURI KIASI CHA KUKURIDHISHA, KWA NINI USIMPE KIBALI CHA KUWA BI MDOGO????

Domo la Mswahili

No comments:

Post a Comment