Dec 22, 2013

NI SAHIHI KUMTEMBEZA UCHI MPENZI WAKO UNAPOMFUMANIA ILI KUMKOMESHA??? INGEKUWA WEWE JE??


Mswahili mwenzangu, ni kweli kuwa kila mmoja ana mtazamo wake na upeo wake wa kufikiri lakini katika hili wacha niseme kuwa Mtazamo huu siuungi mkono hasirani.
 
Kumekuwa na katabia kuwa wapenzi (hasa wa kike) wanapofumaniwa KUTEMBEZWA UCHI HADHARANI ili KUWAKOMESHA.
Ninachojiuliza ni kwamba inakuwaje wewe unayemtembeza mwenzako hadharani kama ingekuwa wewe ndiye uliyekutwa , UNGEKUWA TAYARI KUTEMBEA HADHARANI UCHI????

Mi nadhani kuna ADHABU nyingi ambazo mwenza wako unapomfumania unaweza kumpa kama moyo wako kweli umeshindwa kuvumilia tukio na aibu ile.

ADHABU nzuri kuliko zote ni KUAMUA KUACHANA NAE KABISAA, sidhani kama utaamua kuachana naye kuna aibu ambayo itaendelea kukuzonga mbali na yeye mwenyewe ambaye ataendelea kuzongwa na aibu hiyo milele na milele.

Mswhili mwenzangu JAHAZI LA MSWAHILI linawapa pole wale woote ambao wamepata kufikwa na ADHABU za namna hiyo kwani ni kinyume pia na haki za kibinadamu, unayemtembeza hadharani ni wazi kuwa hatakuwa na hamu ya kuendelea KUISHI ASILANI…..Kwanini adhabu yako ipelekee kuondokewa na uhai kwa yule ambaye dakika chache zilizopita ulikuwa Ukimthamini an kumpenda kwa kila hali?????

maoni yako ni muhimu msomaji wangu….

No comments:

Post a Comment