MCHANO wangu unawahusu wadada
ambao wako skuli lakini mavazi na mienendo yao haiendani na uhusika huo.
Utamkuta mwanafunzi katika
sare za shule lakini alichokivaa ni BALAA TUPU. Mtoto wa kike amevaa sketi
ambayo kama angechaguliwa eneo la kuwapo na
kivazi hicho labda ni baa ambako angekuwa anafanya UBAAMEDI. Mtoto wa watu
amekuvalia Kishati bila shaka kwa wazee wetu walioingia jijini wiki hii toka
mkoani watakwambia ni Kishati cha mdogo wake lakini wapi ni cha kwake!
Mwanafunzi huyo haishii hapo, anapaka kitu cha kumeremetesha mdogo wake kiasi
kwamba UKIKUTANA NAYE hutakuwa na haja ya KUJIULIZA huyu si mwanafunzi
kimaadili bali ni JITU ZIMA LINALOJIUZA kupitia KIVULI CHA UANAFUNZI.
SWALI LANGU; Nyakati zote
niwaonapo wanafunzi wa namna hii hujiuliza Maswali haya
a)
Mwanafunzi wa
namna hii asubuhi ya siku hii ametoka nyumbani kwa wazazi wake au atakuwa
ametoka kwa bwana??? Kama ametoka kwa Mzazi basi ni haki kusema mzazi huyo
hamtakii Mema mtoto wake NA kama atakuwa ametoka kwa bwana basi bwana huyo
atambue kuwa kama alivyofanikiwa yeye kumnasa KINDA huyo na kumuweka ndani
usiku kucha basi siku inayofuata atanaswa na mwenzake anayependa KINDA hilo tunaloambiwa
ni taifa la kesho.
b)
Inakuwaje kwa
walezi wa kule aendako (walimu). Ninastaaajabu kuona kuwa pamoja na kuvaa
katika misingi ya namna ile lakini mwanafunzi huyu bado anaruhusiwa kuingia
shuleni na kupatiwa elimu ambayo TUNADAI ndio MSINGI WA MAISHA YAKE.
ANGALIZO:
Kama tuna nia njema na kizazi chetu kijacho HATUNA BUDI
kuchukua hatua za Makusudi dhidi ya tabia za nama hii. VINGINEVYO;
tutawalalamikia Makondakta, walimu, maofisa na wadau wengine kuwa WANATUHARIBIA
KIZAZI CHA KESHO. Cha msingi, kila mmoja katika nafasi yake ahakikishe
ANACHUKUA HATUA kupambana na hali hii Mzazi, Mwalimu, Mwanajamii.
MSWAHILI NAFUNGA
DOMO LANGU MIE LAKINI UKWELI NDIO HUOOOOO
Ukiwa na CHANO wako niandikie ngogoshakur@yahoo.com
No comments:
Post a Comment